Siasa za kiafrika zimejaa kangaja. Mzalendo mmoja anapoingia katika mfumo wa siasa kama Rais, anabaini kile kinachowafanya viongozi wengi kutofanya lolote la maana katika kuziendeleza nchi zao. Anachobaini ni kuwa, nchi yake ilishauzwa kwa siri na watangulizi wake. Mikataba aliyokabidhiwa inamnyima uhuru, anapoamua kubadili mfumo kwa jeuri, anajikuta katika kivumbi cha kutaka kuuawa. Atafanya nini angali kaapa kutumika, na nchi yenyewe ni miliki ya taifa la Amerika kwa siri? Sasa ni moja tu linamkabili, kifo ama akubali kuiibia nchi yake mwenyewe.
Kitabu hiki ni cha kwanza katika mfululizo wa vitabu Vitatu kuhusu kadhia hii ya kisiasa.