ebook img

Kuwa Mwafrika: Kugundua tera Njia za sili za (Utu) Unhu-Ubuntu-Botho na Kuwa Binadamu PDF

148 Pages·2008·5.039 MB·Kiswahili (Swahili)
Save to my drive
Quick download
Download
Most books are stored in the elastic cloud where traffic is expensive. For this reason, we have a limit on daily download.

Preview Kuwa Mwafrika: Kugundua tera Njia za sili za (Utu) Unhu-Ubuntu-Botho na Kuwa Binadamu

JIUNG B5310. Hisia magi a Mwafrika / Mand Kuibundazit i Unhu-U Mandivamba Rukuni BOOK SERIES NO. 53 Zlio Kuwa Mwafrika Mandivamba Rukuni BOOK SERIES NO. 53 Vitabu vya CASAS vya Kimfululizo vinachapishwa na Kituo cha Masomo Pevu ya Afrika Oradha kamili ya anwani za Vitabu vya Kimfulilizo itapatikana nyuma ya kitabu Kuwa Mwafrika Mandivamba Rukuni Centre for Advanced Studies of African Society kaa £3)IC P.O. Bos 359 Rondebosch, 7700 0 DIE | R S k Cape Town South Africa Ja wA O 2008 Mandivamba Rukuni ' Kilichapishwa kwa mara ya kwanza 2008 CASAS Afrika ya Kusini ISBN 978-1-920294-48-9 Haki zote zimefungwa. Huruhusiwi kuchapisha tena, kuhifadhi kwa hali ya kutumiwa, au kutuma kwa umbo au kwa njia yoyote, kielektonika, kimekanika, kunakilisha, kurikodi, au kwa namna yoyote ile, bila ruhusa ya mwenye haki ya uchapishaji. Chapisho hili lilitolewa kwa msaada mkubwa kutoka W.K. Kellogg, Norad na OSISA Kimepigwa chapa na kufungwa na Kampuni ya Kimawasiliano ya Mega Digital, Afrika ya Kusini Kimetafsiriwa kwa Kiswahili na Martha Oorro Kitabu hiki ni kwa heshima ya wazazi wangu, familia yangu, ukoo wangu wa Rozvi, na heshima ya pekee kwa mizimu ya Waafrika, ambao busara zao tunazihitaji sana sasa, ili kuijenga tena nchi yetu, Afrika SHUKRANI Kuna watu wengi toka ujana wangu hata leo waliosaidia kunifanya nilivyo, na kwa hivyo wametengeneza ufahamu huu wa asili kuwa seti ya mawazo yaliyopangika. Ninawashukuru sana na kwa kweli mpo wengi sana kuweza kuwakumbuka na/au kuwataja kwa majina. Namshukuru Reinhild Niebuhr kwa kunitia moyo na imani yake juu ya kitabu, na baadaye kwa kuhariri mswada. Mandivamba Rukuni UHUSISHAJI NA KANUSHO Profesa Mandivamba Rukuni kwa sasa ni Mkurugenzi wa Kanda wa W.K. Kellogg Foundation Afrika Programme, na kabla ya hapo alikuwa ni Profesa wa Kilimo Uchumi chuo kikuu cha Zimbabwe. Mawazo yote na yaliyomo katika kitabu hiki, hata hivyo, ni ya mtunzi kama mtu binafsi na si lazima yaakisi mawazo ya taasisi ambazo mtunzi alihusika nazo. DIBAJI Ka cha Profesa Mandivamba Rukuni, Kuwa Mwafrika inawasilisha wito muhimu wa kuamsha Waafrika, kurudisha kumbukumbu zao za pamoja utamaduni na kuzitumia kama njia ya kwenda mbele kwenye maendeleo na usasa. Bado sijaona kitabu kingine, ambacho kwa udhahiri, maneno machache na bila madoido ya isimu za lugha au maneno mengi, inalenga na kufanikiwa kubainisha na kutoa uchambuzi mkubwa wa matatizo ya Afrika. Mawazo yaliyoelezwa hapa, hata hivyo, siyo tu uchambuzi unaoweka mambo wazi, bali yanakwenda mbali zaidi ya hapa, na kutoa suluhu na majibu kwa matatizo yanayotukabili kama Waafrika. Kusema kweli, kuwepo kwa kitabu hiki kumeniondolea kabisa mashaka akilini mwangu kuwa, sasa tunapata matumaini juu ya wazo la Mwamko wa Kiafrika. Ujumbe wa Mandivamba Rukuni ni kuwa lazima turudi tena kwenye mizizi yetu, na kuokoa vizuri vilivyopo na vya kufaa kutoka huku, na kuvitumia kama msingi wa kwenda mbele. Kwa kiasi kikubwa ipo kwenye kiini cha wazo la Kiafrika la Sankofa (Sankofa ni neno la Kiakan inayomaanisha kuwa, “lazima turudi nyuma na kuyaelewa na kuyaokoa/kuyarudisha katika hali nzuri maisha yetu yaliyopita ili tuweze kwenda mbele; ili tujue kwanini na kwa namna gani tumekuwa tulivyo leo.”). Kitabu hiki, ambacho kimejikita kifalsafa kwenye dhana ya Unhu-Ubuntu-Botho, kinatambua sifa za jumla na za kiutu za wazo hili na maadili yake. Inakumbatia utu kwa ujumla, wakati ikiweka kukumbatia huko kwenye msingi wa ukombozi wa Kiafrika kwa taaluma ambayo inasherehekea bila kufifisha chanzo chake. Kitabu hiki kimetoka ni kwa wakati muafaka kwa sababu kinakuja wakati wa historia, ambapo Waafrika wametingwa na mashaka huku wakiandamwa na hali ya kukata tamaa. Mizimu ya Rozvi inaongea kupitia kwa Rukuni na ujumbe wao ni sauti kubwa na wa kueleweka.

See more

The list of books you might like

Most books are stored in the elastic cloud where traffic is expensive. For this reason, we have a limit on daily download.